Surah Al-Infitar ( The Cleaving )

Swahili

Surah Al-Infitar ( The Cleaving ) - Aya count 19

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ ﴿١﴾

Mbingu itapo chanika,

وَإِذَا ٱلْكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتْ ﴿٢﴾

Na nyota zitapo tawanyika,

وَإِذَا ٱلْبِحَارُ فُجِّرَتْ ﴿٣﴾

Na bahari zitakapo pasuliwa,

وَإِذَا ٱلْقُبُورُ بُعْثِرَتْ ﴿٤﴾

Na makaburi yatapo fukuliwa,

عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ ﴿٥﴾

Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.

يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلْكَرِيمِ ﴿٦﴾

Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

ٱلَّذِى خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ ﴿٧﴾

Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,

فِىٓ أَىِّ صُورَةٍۢ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ ﴿٨﴾

Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.

كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ ﴿٩﴾

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَٰفِظِينَ ﴿١٠﴾

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,

كِرَامًۭا كَٰتِبِينَ ﴿١١﴾

Waandishi wenye hishima,

يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ ﴿١٢﴾

Wanayajua mnayo yatenda.

إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍۢ ﴿١٣﴾

Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,

وَإِنَّ ٱلْفُجَّارَ لَفِى جَحِيمٍۢ ﴿١٤﴾

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;

يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ ٱلدِّينِ ﴿١٥﴾

Wataingia humo Siku ya Malipo.

وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَآئِبِينَ ﴿١٦﴾

Na hawatoacha kuwamo humo.

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ ﴿١٧﴾

Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

ثُمَّ مَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ ﴿١٨﴾

Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌۭ لِّنَفْسٍۢ شَيْـًۭٔا ۖ وَٱلْأَمْرُ يَوْمَئِذٍۢ لِّلَّهِ ﴿١٩﴾

Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.